TVZ :: Taarifa ya Habari


TVZ :: Habari za Kitaifa

Dk. Shein Achukua Fomu Kuwania Urais wa Zanzibar Kupitia CCM - 18 Aug 2010

MGOMBEA wa urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk Ali Mohammed Shein amechukuwa fomu kuwania nafasi ya Uraisi wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM

Mara baada ya kucukua fomu Dr. Shein pamoja na waliomshindikiza walielekea katika ofisi ya CCM Mkoa wa Mjini Magharibi kwa ajili ya sughuli za kutafuta nwadhamini. Akiwa katika ofisi hiyo alisema hakuna mbadala wa chama cha CCM hivyo wanachama wana kila sababu ya kuongeza nguvu ili kukipatia ushindi chama chao katika uchaguzi mkuu ujao.

Aidha alisema bila ya wanachama wa CCM kushirikiana na kuwa kitu kimoja ushindi hautaweza kupatikana kwa kuwa msingi ya ushindi ni kuunganisha nguvu na kuachana na makundi ambayo nayaweza kudhoofsisha nguvu za chama. Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imeweka mwisho wa kurejesha fomu hizo ni Agosti 30 mchana zikiwa imeambatanishwa na shilingi millioni mbili taslamu na wadhamini mia mbili kwa mikoa mitano ya Unguja na Pemba.

Hadi sasa waliochukua fomu kuwania nafasi ua uraisi wa Zanzibar ni fomu ni pamoja na Maalim Seif Sharif Hamad, (CUF), Juma Ali Khatib TADEA, Haji Ambar Khamis NCCR-Mageuzi na Said Soud Said wa Chama Cha Wakulima (AFP).




Dk. Shein Ahidi Kuwatumikia Wanzanzibari Kwa Uwezo Wake Wote - 17 Aug 2010

MGOMBEA wa urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk Ali Mohammed Shein amewataka wana CCM kusafisha nyoyo zao na kuondokana na chuki na ubinafsi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba 2010. Dk Shein ameyasema hayo jana katika hoteli ya Bwawani wakati akizungumza na wagombea wa nafasi mbali mbali za ubunge, uwakilishi na udiwani walioshinda na walioshindwa katika mchakato wa upitiaji majina ya wagombea uliofanyika hivi karibuni Mjini Dodoma
Amewaahidi wanachama hao kwamba chini ya uongozi wake iwapo atakingia madarakani atahakikisha anaendesha nchi kwa kufuata misingi ya haki, utawala bora, upendo na maelewano huku akisisitiza suala la nidhamu kwa watu wote kwa kuwa huo ndio msingi madhubuti wa kuendeleza maelewano miongoni mwa jamii ya wazanzibari.




Zanzibar Minister Advocates ICT Application - 14 Aug 2010

Zanzibar deputy minister for Communication, Culture and Sports Mahmoud Thabit Kombo has said that information and communications technology (ICT) is still lagging behind in Unguja and Pemba despite having contributed a lot to the Isles’ economic growth and employment. He made the remarks yesterday at the 10th anniversary since Zanlink company was launched at Shangani in Unguja. He said many people thought it was the government’s responsibility to improve the sector, adding that it also included the private sector which carried a lot of weight in developing the country. “It is the people’s prerogative to improve the ICT sector and it is imperative that local investors come forward to help us in this,” he said.


“We are currently planning to improve our services so that we become the best company here and in Africa with a view of contributing to the economy and eradicating poverty,” he said. He explained that a total of 900 people benefited from their services and they planned to reach out Unguja and Pemba. He said the ICT sector was vital in developing the tourism sector and that’s why the company planned to broaden its services in the Eastern Zone in Zanzibar where there were many tourist projects.



TVZ :: Habari za Uchumi na Biashara

Isles Tourism Sector Loses Billions

ERNST and YOUNG company of Dar es salaam has been hired to investigate monetary losses in the tourism sector in Zanzibar, the Minister for State, Finance and Economic affairs, Dr Mwinyihaji Makame Mwadini, informed the House here on Thursday. ''In our programme to improve revenue collection, we have hired the company to study why there have been revenue losses in the tourism sector,'' Dr Makame told the House when moving a motion for the 93.6bn/- budget proposal for his ministry for 2010/2011.
He said that the study aimed at controlling tax evasion, and improving collection targeting 117bn/- in 2010/2011. The minister said that a study on the appropriate methods in tax collection had been conducted by the TRA in collaboration with the Economic Research Bureau of the University of Dar es Salaam. He said that the findings have been forwarded to the government. Dr Makame told the House that his ministry would also improve awareness campaign dubbed 'TEKNOHAMA communication strategy' so that tax payers refrain from evasion in the islands.

''We have also planned to review all tax exemption regulations in efforts to control the misuse of opportunity. Any dishonest people who would be discovered cheating will not have any exemption or risk tax exemption nullification,'' the minister said. He said that the Zanzibar Revenue Board (ZRB) collected 89.3bn/- last year instead of the targeted 96bn/-, while Tanzania Revenue Authority (TRA) managed to collect only 60bn/- against target of 63.2bn/.




Hoteli Tatu Zateketea Kwa Moto Jambiani

JUMLA ya hoteli tatu za kitalii na zaidi ya nyumba sita za wananchi zimeteketea kwa moto jana asubuhi katika kijiji cha Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wananchi wa kijiji hicho walioshuhudia moto huo wamesema waliona moto mkubwa ukiwaka katika hoteli za kitalii na kutoka nje na kusaidiana na wamiliki wa hoteli hizo kwa kuuzima.Hoteli zilizoungua ni pamoja na Visitors Inn, Sau Inn na Bungalow ambapo zote zipo eneo la Jambiani ukanda wa pwani ambapo moto huo uliwaka kwa kasi kutoka na hoteli hizo kuezekwa kwa makuti ambapo moto ilishika kasi kutokana na upepo mkubwa uliokuwa ukivuma nyakati za asubuhi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Augustine Olomi amesema amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la moto na kuunguza hoteli za kitalii na nyumba zilizo karibu na hoteli hizo. Kamanda huyo amesema hadi sasa thamani kamili ya vitu vilivyoungua ndani ya hoteli hizo pamoja na nyumba zilizo karibu na hoteli bado haijajulikana thamani yake lakini zimeteketea kwa kiasi kikubwa. Katika hoteli ya Visitors inn zaidi ya vyumba 12 vya kulalia wageni na sehemu ya mkahawa zimeteketea kwa moto huo huku baadhi ya vitu vikiwa vimeteketea kwa kiasi kikubwa hasa katika maeneo ya jikoni na kumbi za hoteli hiyo.



TVZ :: Habari za Burudani na Michezo

ZFA KUviadhibu Vilabu vya Soka

Chama Cha Soka Zanzibar (ZFA) kimesema hakitovumilia kuviadhibu vilabu vinavyoleta vurugu na kupiga waamuzi viwanjani ikiwa pamoja na kufungia wachezaji na viongozi ili kuvifanya viwanja vya michezo kuwa ni sehemu ya burudani.Kauli ya ZFA imekuja baada ya tukio la wiki iliyopita timu ya New Boko kudaiwa kumpiga mwamuzi hadi kuzirai katika mchezo wa kupanda daraja la kwanza.Katibu Mwenezi wa ZFA, Maulid Hamad Maulid amethibitisha kupokea taarifa za waamuzi na Kamisaa wa mchezo ambapo Kamati Tendaji itakaa wakati wowote kuanzia sasa ili kulijadili tukio hilo
Kauli ya ZFA imekuja baada ya tukio la wiki iliyopita timu ya New Boko kudaiwa kumpiga mwamuzi hadi kuzirai katika mchezo wa kupanda daraja la kwanza.
Katibu Mwenezi wa ZFA, Maulid Hamad Maulid amethibitisha kupokea taarifa za waamuzi na Kamisaa wa mchezo ambapo Kamati Tendaji itakaa wakati wowote kuanzia sasa ili kulijadili tukio hilo. Amesema inssikitisha kuona vitendo vya kihuni vikijitokeza viwanjani na kugeuza viwanja sehmu za mapambano badala ya burudani na hivyo kutia dosari mchezo huo wa soka unaopendwa na wengi.

“Tunaendesha Soka kwa kanuni ambazo zinaendesha mchezo huu na kila timu zinzoshiriki mashindano tunasimamia “ Alisema Maulid.
Amesema kifungu ch 24 na 25 cha kanuni za mashindano vinaeleza na adhabu kwa timu zinazofanya fujo viwanjani na zinazosababisha mchezo kuvunjika kabla ya mchezo ambayo vitatumika. Inadaiwa siku ya mchezo huo mwamuzi Ramadhan Kibo alipigwa na mchezaji Omar Haji wa New Boko kabla ya kuvamiwa na kundi la wachezaji wenzake na baadaye kupigwa kichwa na amashabiki hali iliyosababisha azirai na kuokolewa na wasamaria.




Maulid Ashindwa Kugombea Ubunge

KATIBU Mwenezi wa Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) Maulid Hamad Maulid amesema tuhuma zinazomkabili za kupandikizwa kumshambulia mwizi kwa panga ndizo zilizomfanya ashindwe kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Jang’ombe kama alivyopanga awali.Maulid alitoa ufafanuzi huo alipohojiwa Mjini hapa kufuatia kuvuma habari za Katibu huyo na kutangaza kuwa anagekuwa miongoni mwa wagombea ambao wangeingia katika mchakato huo kupitia Chama cha Mapinduzi(CCM).

KATIBU Mwenezi wa Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) Maulid Hamad Maulid amesema tuhuma zinazomkabili za kupandikizwa kumshambulia mwizi kwa panga ndizo zilizomfanya ashindwe kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Jang’ombe kama alivyopanga awali.



TVZ :: Habari za Kimataifa

Zanzibar Kutumia Sub-marine Cable Kwa Mawasiliano

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema imo katika mchakato wa uwekaji waya chini kwa chini kwa ajili ya mawasiliano ya simu ili kuwawezesha wananchi kupata huduma ya mawasiliano kwa urahisi zaidi.Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Wizara ya Utalii, Biashara na Uwekezaji Samia Suluhu Hassan alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Bwawani Mjini Unguja kuafuatia ziara yake ya nchini China.

Alisema kuwa hatu hiyo pamoja na huduma hiyo kuwafikia wananchi lakini pia ni mateghemeo yao kuwa wataifikisha hadi katika sehemu zote za Serikali ya Zanzibar kwa manufaa ya kuondokana na hali ya usumbufu wa mawasiliano. Samia alisema kuwa katika kufanikisha hilo tayari Serikali ya Zanzibar kupitia ujumbe uliotembelea nchini China hivi karibuni akiwamo Rasi Amani Karume, wamefanya mazungumzo na Kampuni mbili nchini humo na kuahidi kufanya kazi hiyo.




ADB Yaridhishwa na Miradi ya Zanzibar

BENKI ya Maendeleo Afrika (ADB) imeeleza kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa hapa Zanzibar kwa ushirikiano baina ya Zanzibar na Benki hiyo na kuahidi kuendelea kuunga mkono juhudi hizo ili kuleta mafanikio zaidi. Mwakilishi Mkaazi wa Benki ya Maendeleo Afrka (ADB), anaemaliza muda wake hapa nchini Dk. Sipho Moyo aliyasema hayo leo wakati alipokuwa na mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume, Ikulu mjini Zanzibar.

Katika maelezo yake Mwakilishi Mkaazi huyo, alimueleza Rais Karume kuwa ADB inafarajika kwa kiasi kikubwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyopo hapa Zanzibar kutokana na kuweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa. Alisema kuwa hatua ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa mashirikiano na ADB hapa Zanzibar ni nzuri na ya kuungwa mkono katika suala zima la kuleta maendeleo na kuimarisha uchumi. Dk. Moyo alisema kuwa kutokana na hatua hizo ADB itaendeleza kuunga mkono zaidi miradi iliyopo na kuiimarisha ile inayoanzishwa kutokana na kuwa na mwanga wa mafanikio.